ILIPOISHIA,
Braison aliitwa na Nesi ili kupokea majibu ya vipimo …
SONGA NAYO…
Mwili mzima ukiwa unamtetema, Nesi alimwambia,
“Relax…” Nesi alimwambia
Kwa umakini mkubwa sana, alitulia kama maji ya mtungi huku Nesi akiwa ameshika kalamu.
“Hongera kwa hatua hii.” Nesi alimwambia.
“Majibu yakoje?” Alimuuliza.
“‘Uko vizuri kikubwa endelea kuwa muaminifu kwenye ndoa na zingatia kutumia kinga”
Braison alishusha pumzi na kuachia tabasamu kisha akatoka chumbani humo.
Baada ya dakika kama 1 hivi, Sarah aliitwa kisha akaingia ndani na kupatiwa majibu.
Katika majibu hayo, vipimo vilionesha yuko salama huku akiwa na ujauzito wa wiki 3.
‘” Hongera uko salama na tayari mpaka sasa wewe ni mama kijacho “
“Waohhh…!, kweli ?” Alimuuliza kwa mshangao.
“Vipimo vinaonesha hivo zingatia mlo kamili lakini pia utaanza kuhudhuria clinic”
“Asante…”
Sarah alitoka chumbani humo akiwa na tabasamu kisha akaambatana na mme wake kuelekea nyumbani.
” Mme wangu mambo yameiva sasa. Tumesubiri kwa mda mrefu sasa hatimaye ombi letu limejibiwa…” Sarah alimwambia kwa tabasamu.
“Kwakweli nina furaha isiyo na kifani . Leo lazima tuchinje kuku maana nilikuwa sijisikii vizuri kukosa mtoto..”
” Hahaha, lakini mme wangu mbona ulikuwa unaogopa kupima” alimwambia huku akiachia cheko laini
“‘Hahaha hapana bwana ebu tuongee mengine”
Baada ya mazungumzo hayo, waliendelea na safari na walipofika nyumbani, jogoo mkubwa alimwagwa damu na kukaushwa.
Ni furaha iliyokuwa ya aina yake kwa wawili hao.
Baada ya mambo kuwa mazuri, utaratibu wa kwenda clinic kila mwezi, ulianza, mpaka ilipotimia miezi 9.
Cha kushangaza, baada ya miezi 9 kutimia, Sarah alienda hospitali kujifungua lakini uchungu hakuwa nao ndipo alipokaa wodini kwa wiki moja bila kujifungua.
Maneno ya chinichini yalianza kusambaa mtaani mara baada ya Sarah kushindwa kujifungua.
Daktari alimfanyia vipimo kuona kama anaweza kufanyiwa upasuaji lakini cha kushangaza, mtoto alionekana bado mchanga yaani hajatimiza mda wa kuzaliwa.
Sarah alipewa taarifa hiyo kisha akaambiwa arejee nyumbani.
Alirejea nyumbani huku tumbo likiwa limetuna kweli.
“Mke wangu kulikoni?” Braisona alimuuliza mke wake.
“‘Nimeambiwa mda haujafika….”
“Hee!, mbona miezi 9 tayari?”
” Nami nashangaa lakini yatupasa kufuata maelelezo ya daktari..”
Maisha yaliendelea hivohivo mpaka hapo alipotimiza miezi 15 ndipo alipohisi uchungu.
Ilikuwa ni mida ya saa 4 za usiku hivi, ndipo hali ya Sarah ilipobadilika huku uchungu ukiongezeka.
Braison alimbeba mkewe kwenye baiskeli kisha akampeleka hospitali.
Baada ya kufika, walimpokea kisha akakimbizwa kwenye wodi ya kinamama wajawazito.
Ndani ya mda mfupi, Nesi alianza shughuli ya kumsaidia kujifungua huku kwa pembeni akiwa na mwenzake kujua ni mtoto gani ambaye amemaliza miezi 15 ?
0 Comments